Uchaguzi Serikali za Mitaa: Wilaya ya Kinondoni yatoa maelekezo
Msimamizi wa uchaguzi Wilaya ya Kinondoni ametoa maelekezo kwa wananchi na wagombea kutakiwa kuyazingatia.
Akizungumza na Global Publishers, msimamizi Kiduma Siga Mageni alisema kuwa, maelekezo hayo tayari yameshabandikwa kwenye ofisi za maofisa watendaji wa Kata zote za Wilaya ya Kinondoni.
“Ni wajibu wa kila mwananchi na mgombea kwenda kwenye ofisi za afisa watendaji kuangalia maelekezo kuhusu uchaguzi kama mtu una vigezo vya kugombea. Maelekezo hayo tayari yameshabandikwa katika ofisi zote za maofisa watendaji wa Manispaa ya Kinondoni,” alisema. Uchaguzi huo wa wenyeviti wa mitaa unatarajiwa kufanyika 24/11/2019.
Imeandaliwa na Neema Adrian/ GPL
Comments are closed.