The House of Favourite Newspapers

Uchaguzi wa Rais Kenya Huenda Ukaahirishwa

0
Uhuru Kenyatta.
UCHAGUZI wa marudio wa urais nchini Kenya huenda ukaahirishwa kutoka tarehe 17 mwezi ujao.
Tume ya Uchaguzi na Mipaka, IEBC, imekuwa ikikutana kuangalia uwezekano wa kuahirisha Uchaguzi huu baada ya kampuni ya Ufaransa ya Safran Morpho kuomba muda zaidi kuboresha mitambo inayotumiwa kuwatambua wapiga kura.
Raila Odinga.
Mbali na hilo, Muungano wa Upinzani Nasa, unaoongozwa na Raila Odinga, umesema Uchaguzi hautafanyika iwapo marekebisho hayatafanyika ndani ya Tume ya uchaguzi ikiwa ni pamoja na kujiuzulu kwa Ezra Chiloba Mkurugenzi Mkuu wa Tume hiyo.
Chama cha Jubilee cha rais Uhuru Kenyatta kinashutumu shinikizo hilo la upinzani na kusisitiza uchaguzi ufanyike kama ulivyopangwa.

JWTZ Wakizika Miili ya Watoto Waliolipukiwa Bomu Monduli

Leave A Reply