Uchumi Wetu Kiboko, SADC Yaimwagia Tanzania Sifa – Video
Kauli hiyo ameitoa wakati wa kuanza kwa mkutano wa SADC unaofanyika jijini Dar es salaam, ambapo viongozi mbalimbali wa jumuiya hiyo, wakiwemo viongozi wastaafu na mawaziri, wamehudhuria.
“Uhimilivu wa uchumi ni nyenzo muhimu katika maendeleo, nchi wanachama zimekidhi vigezo vya SADC kiuchumi, takwimu zimeonesha Tanzania inafanya vizuri, na kwa vigezo pekee Tanzania ndiyo nchi pekee ambayo imefikia ukuaji wa asilimia saba, hivyo mjipongeze.
“Katika kufikia uchumi wa viwanda, nchi wanachama hawana budi kukuza uzalishaji wa umeme, kwa kuwa ni kitu muhimu kwenye ujenzi wa viwanda. Nashukuru katika wiki ya viwanda iliyopita hivi karibuni, tumeshuhudia kuzinduliwa kwa mradi mkubwa wa umeme katika maporomoko ya mto Rufiji ambao ujenzi wake unaendelea,” alisema.
FUATILIA MKUTANO HUO HAPA
Comments are closed.