Ujumbe wa Mpoto Wahusishwa na Baa la Njaa
Mrisho Mpoto akiwa Global Tv Online
Mwanamuziki wa Muziki wa Asili Bongo na mtumbuizaji kwa staili ya kughani mashairi, Mrisho Mpoto ameandika ujumbe mzito katika mtandao wa instagram unaosomeka
“Wakati wewe unasema mwanamke Malaya apigwe mawe, basi wewe usiyekua na dhambi njoo uwe Wa kwanza kumpiga mawe!!” aliandika hivyo Mrisho Mpoto.
Mrisho Mpoto watatu kutoka kushoto akiwa katika matembezi kupinga ujangili.
katika majadiliano waliyochangia hoja hii watu ishirini ambapo walitoa maoni yao na kuhusisha na ugumu wa maisha, baa la njaa na ukosefu wa mvua nchini. ambapo mchangiaji huyo aliandika hivi…
“Tunahukumiana ndio maana mvua hazinyeshi na baa la njaa linatikisa nchi” Aliandika hivyo mchangiaji huyo.
Mrisho Mpoto
Aidha, Mpoto ambaye amewahi kuwa balozi wa amani nchini, wiki mbili zilizopita alipata mualiko kutoka ubalozi wa China katika hafla ya kupinga ujangili nchini na kwingineko, Mpoto anatajwa kama ni msanii mwenye kutetea haki za binadamu na wanyama.
Picha na Ujumbe wa Mrisho Mpoto Instagram
Salum Milongo/GPL
Comments are closed.