The House of Favourite Newspapers

Unafiki Ndiyo Utamfukuzisha Kazi Omog

0
Kocha wa timu ya Simba, Joseph Omong.

‘OMOG afuku­zwe’, ‘Omog abaki’, ‘Omog hatufai’, ‘Omog ni tatizo’, ‘timu haziche­zi vizuri tatizo ni Omog’.

Hizo ni baadhi ya kauli ambazo zimekuwa zikita­wala kwenye vyombo vya habari, mitandaoni, kwenye vijiwe na kwingine kote am­bapo kuna mazungumzo kuhusu Klabu ya Simba.

 

Simba ipo katika nafasi ya nne ikiwa imezidiwa pointi mbili na Mtibwa Sugar am­bayo inashika usukani katika Ligi Kuu Bara, pointi za Simba ni sawa na zile za wapinza­ni wao wa jadi, Yanga, wote wakiwa wameshinda michezo miwili na kupata sare mbili.

 

Ubingwa unawaniwa na timu zote lakini Simba kunaweza kuwa na presha kubwa zaidi ya timu nyingine zote kutokana na mazingira halisi ya timu hiyo hasa ni kutokana na kutumia ki­wango kikubwa cha fedha ka­tika usajili, pili ni kiu ya kuu­taka ubingwa wa ligi hiyo baada ya Yanga kutawala kwa miaka kadhaa.

 

Omog ame­wahi kuipa ub­ingwa Azam FC, pia ndiye aliyei­wezesha Simba kupata nafasi ya kurejea ka­tika michuano ya kimataifa, kwa wasifu wake katika soka la Afrika sina shaka na uwezo wake wa kufundisha hasa ukizingatia aina ya mazin­gira ambayo anafundishia.

Kikosi cha timu ya Simba.

 

Siyo lazima kocha bora afan­ikiwe katika kila timu anayo­fundisha lakini kuna wakati in­ategemea na mahitaji ya pande mbili, hapo namaanisha kocha anahitaji nini na kwa muda gani na pili ni uongozi nao una­hitaji nini na kwa muda gani.

 

Katika kundi la pili wakati mwingine huwa linaongozwa na munkari wa mashabiki wao, mara nyingi mashabiki wanaweza kuwa na nguvu kubwa ya kushinikiza jambo fulani lifanyike na likafanyika kweli hata kama halikutakiwa kufanyika kwa wakati huo.

Omog ni kocha anayejielewa, amekabidhiwa timu ya msimu huu ikiwa ‘mpya’, nasema hivyo kutokana na aina ya usajili uliofanyika wakati msimu ukikaribia kuanza, ndi­yo alipata muda wa kuwa na wachezaji kwa wiki kadhaa na hiyo ikamsaidia kuwajua na alitakiwa kupanga mipango yake kulingana na mahitaji ya timu na yaendane kwa wakati.

 

Usajili uliofanyika huku vyombo vya habari viki­tumia nguvu kuwapamba wachezaji hao, kumewafanya mashabiki waamini Simba ina haki ya ushindi katika mechi zote, kinyume cha hapo ko­cha atakuwa hana msaada.

 

Nikukumbushe, Real Ma­drid iliwahi kuwa na kikosi cha mastaa wengi miaka kad­haa iliyopita, makocha wengi walishindwa kupata mafani­kio makubwa kipindi hicho kutokana na presha na ku­kosa mtiririko sahihi wa ku­waunganisha mastaa hao.

 

Wiki kadhaa zilizopita nil­iandika makala katika kolamu hii nilieleza, Simba wanatakiwa kuwa makini katika kuwafanya mastaa wao kuwa wamoja, kuwa na wachezaji mastaa na kuwafan­ya wacheze kitimu ni vitu viwili tofauti.

 

Simba ya sasa inahi­taji umoja na kumpa nafasi kocha afanye kile anacho­fanya ili ak­ishindwa basi ahukumiwe kwa kile ambacho k i t a o n e k a n a uwanjani, tak­wimu hazidan­ganyi, soka ni mchezo wa takwimu pia.

 

Katika soka kuna kitu ki­naitwa ‘chem­istry’ yaani mu u n g a n i k o wa kuelewa­na baina ya mtu mmoja na mwingine, mfano Haruna Niyonzima ak­ishika mpira anajua fulani ataelekea wapi au atafanya nini, hivyo chemistry kuna wakati huwa haipatikani kwa haraka.

 

Najua hizi kelele hazijatoka nje ya Simba tu, bali kwa asili ya soka letu lilivyo, kuna watu kutoka ndani ya Simba yenyewe ndiyo waanzilishi wa presha hiyo na wanachofanya ni ku­seti mitambo tu ili ikikolea basi iwe rahisi kocha kufukuzwa.

 

Moja ya kitu ambacho Mungu ametujalia Watanza­nia ni kuwa wanafiki, huyo anayekuchekea usoni kumbe upande wa pili anakumaliza, ndani ya klabu zetu hizi kubwa huko hayo ndiyo maisha yao.

 

Hata kama Simba wenyewe wanakanusha nahisi mpishi wa kelele zote hizo ameanzia nda­ni ya nyumba yao. Tukumbuke kumfukuza Omog kisha kum­leta kocha mpya hakutamaani­sha ndani ya muda mfupi Sim­ba itakuwa bingwa mapema.

AJIBU Amfungukia Mazito Raphael Kikosini

Leave A Reply