Usiku wa Uswazi watikisa Dar Live
Msaga Sumu akiwachizisha mashabiki waliofurika ndani ya Dar Live.
Juma Nature akiporomosha burudani ya aina yake wakati wa shoo ya Usiku wa Uswazi usiku wa kuamkia leo.
Mamaa wa Chura, Snura akifanya yake stejini.
Staa wa Bongo Muvi, Gabo Zigamba akionyesha ‘machejo’ stejini.
Man Fongo ‘Mzee wa Hauna’ akiwadatisha wapenzi wa burudani Dar Live.
MC Soud mkali wa kibao cha ‘Naipenda Simba’ akiwapa raha mashabiki.
Shabiki akimtunza MC Soud baada ya kumkonga roho.
MKONGWE wa Bongo Fleva, Juma Nature, mkali wa Mduara Snura, mkali wa Mchiriku Msaga Sumu pamoja na mkali wa Singeli Man Fongo usiku wa kuamkia leo wametikisa vilivyo kwa shoo zao kali kwenye “Usiku wa Uswazi” ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live uliopo Mbagala-Zakhem jijini Dar.
Mbali na wakali hao kutoa burudani kali pia kulikuwepo na mastaa kibao kutoka Bongo Muvi wakiongozwa na Gabo Zigamba.
Picha na Richard Bukos / GPL