The House of Favourite Newspapers

Utamu Usioisha Hamu -6

0


ILIPOISHIA JANA…
Alijikuta akizidi kuchanganyikiwa kwa jinsi bibie alivyovutia.Monica alitembea utadhani anaionea huruma aridhi ya Mungu kuikanyaga!. Alijua kutembea kwa maringo, hiki nacho kilimduwaza Saka. Wanaume wengi wamuonapo barabarani lazima wamsindikize kwa macho ya matamanio, ni mzuri hasa.
SASA ENDELEA NA SIMULIZI HII BOMBA…
Kiu kubwa ya mapenzi ilimsumbua Saka, alijikuta akitamani kuwa mwili mmoja na msichana huyo mrembo. Baada ya Monica kupotea upeo wa macho yake, aliondoa gari na kumfuata Seki alipomwacha.

“Seki, bosi wako anatembea na mwanamke mzuri sana…” punde alipokutana na Seki alimwambia.

“Sawa, ila usizungumzie suala la demu wa bosi wangu…achana nalo kabisa…,” Seki alijikuta akimkatisha mazungumzo rafiki yake, alikuwa na sababu ya kufanya hivyo. Kila aliposikia habari hizo moyo ulimuuma. Saka hakuweza kumweleza kile kilichotokea baada ya kuona rafiki yake anakasirika kusikia habari za Monica.Alitaka amwambie amemtongoza na demu anaonekana kuridhia, akahisi huenda angegombana na rafiki yake.

“Mbona unakasirika Seki…eeeh!”

“Sikiliza, nishakuambia…sitaki kusikia unamzungumzia demu wa bosi, huna kingine cha kuongelea?”

“Basi, nisamehe kaka…,” Saka alisema.

Waliachana, Sakala alienda moja kwa moja Ubungo kuendelea na kazi ndogo ndogo gereji, na baadaye alirejea nyumbani kwake. Alikuwa akiishi maeneo ya Ubungo Maziwa, hakujua nyumba anayoishi Monica. Alitamani kuulizia, akahisi huenda angeharibu na Monica angejua asingeweza kumpa kile anachokitaka.

***

Monica alipoingia ndani kwake, hakuweza hata kufanya usafi, alichoka mwili na hivyo alijitupa kitandani kigoigoi na kupitiwa na usingizi. Saa kadhaa alipozinduka, aligundua mumewe tayari alisharudi na alikuwa amejilaza pembeni yake.

“Sweetie, mbona umechelewa…ulikuwa wapi?” Monica alimuuliza mumewe kwa sauti ya uchovu.Ni mwanamke msaliti na mwenye wivu sana kwa mumewe.

“Nilikuwa kazini mke wangu, leo wateja wengi…” Kapesa alidanganya, akili yake ilihama na kwenda katika matukio aliyoshuhudia kwa Samira, mwanamke aliyempenda na kumpangishia chumba kumbe ana mahusiano na mwanaume mwingine jirani yake aitwaye Madenge, ajabu analea mimba ambayo sio yake.Kitu hiki kilimuuma sana.

“Ohooo, sio kawaida yako kuchelewa namna hii, saa hizi saa tano usiku…”

“Ni kweli, sorry my wife…,” alisema Kapesa. Akamkumbatia mkewe, naye mwanamke akamkumbatia. Kila mmoja aliwaza lake kichwani, Monica alikumbuka jinsi Mzee Mombasa alivyompa dozi tamu ya mapenzi hadi kiu kuisha kabisa, hakika alijikuta akitabasamu mwenyewe. Wakati huo, Kapesa aliwaza afanye nini juu ya Samira, amuache au aendelee naye hadi kodi ya nyumba itakapokwisha ndipo amweleze ukweli kuwa hawezi kuwa na mwanamke msaliti. Wazo hili alilipa kipaumbele zaidi, alipanga kumwacha Samira ingawa ni mwanamke anayejua mapenzi na kukata kiu yake.

Asubuhi, Monica alimpelekea mumewe maji ya vuguvugu bafuni, akamfunga taulo.

“Oga basi mume wangu, ukija kuna kitu nataka tuzungumze…”

“Sawa mke wangu, kitu kizuri?”

“Yaah, mkeo lazima aongee nawe kitu kizuri…”

Alimpiga mabusu matatu ya midomoni, Kapesa akaingia bafuni kuoga asubuhi hiyo, hakuchelewa alirejea na kukuta nguo zake zimenyooshwa vizuri. Akavalishwa hadi nguo, hiki ni kitu ambacho kimemfanya azidi kumpenda mkewe kuliko kawaida licha ya kuwa wanaume huwa hawaridhiki na mwanamke mmoja.

Alikuta ameandaliwa rosti ya maini nzuri, akala na kushiba kisha mkewe akamuita chumbani.

“Mume wangu, nakupenda sana…naomba uiboreshe ofisi yako ya saluni…na pia ufungue duka la vipodozi…utafute dada yako aweze kusimamia…umenielewa?”

“Ndiyo mke wangu…” Kapesa alipewa kiasi cha milioni kumi ambazo alishindwa kuelewa zimetoka wapi, kwasababu wazazi wa Monica wana uwezo kidogo, alihisi huenda ameomba pesa kwa wazazi wake.

“Nani amekupa pesa zote hizo?”

“My dady…wazazi wangu wananipenda na hawapendi niteseke,” alidanganya, akimtolea mumewe tabasamu nono!

Zilikuwa pesa nyingi sana, mwanaume alizichukua na kuzigawanya katika mifuko yake ya suruali, hakujua mkewe amehongwa na hawara yake. Alichoamini mkewe ni mwaminifu na anampenda sana. Hakujua mkewe ana uhusiano na wanaume wengine nje ya ndoa.

Kapesa alibeba mkewe juu juu huku akimwambia maneno mengi ya kimapenzi, alimbusu na kumwahidi lazima atafute pesa aweze kupata utajiri.

“Pambana mume wangu, nakutegemea kwa kila kitu…,” alisema Monica.

“Nitapambana sweetie…” Kapesa alisema, waliagana mwanaume akatoka akiwa na furaha na kumwacha mkewe nyumbani.

Njiani wakati anaenda kazini, alishangaa simu yake ikiita, alipoitazama aligundua ni baba mkwe anampigia. Aliipokea haraka, na kumsalimia.

“Shikamoo baba…” alisema Kapesa huku akitamani kumwambia, “Baba nashukuru kwa pesa ulizompa Monica, akaona atulie kwanza.

“Marahabaa mwanangu, za siku nyingi…”

“Salama tu baba…vipi mnaendeleaje?”

“Naumwa kiasi, kifua kinanisumbua sana mwanangu…

“Pole sana baba…”

“Shida yangu kubwa mwanangu, naomba unitumie pesa nikapate vipimo…” Kapesa alishtuka sana, kama baba amempatia mwanaye milioni kumi, halafu ananiomba pesa ya vipimo, inamaana sio aliyempa mke wangu pesa?.

“Unashida na kiasi gani?”

“Nitumie yoyote, ila ikifika elfu hamsini basi…itanitosha…” baba mkwe alisema, Kapesa jasho lilimtoka, sasa akaanza kuingiwa na wasiwasi huenda mkewe anamdanganya, pesa amezipata wapi?

Alimwahidi baada ya nusu saa angemtumia akishuka kwenye daladala, mzee alishukuru sana.

Mawazo mengi yalimtawala Kapesa! “Au mzee ananipima kama naweza kumsaidia, kama amempatia mwanaye milioni kumi, atakosaje shilingi elfu hamisini?” Aliwaza sana.

Ilibidi ampigie mkewe simu baada ya kumtumia baba mkwe pesa!.

“Monica, unajua sielewi…”

“Kwanini?”

“Wee unaniambia wazazi wako wamekupa pesa, milioni kumi…ajabu baba yako ananiomba elfu hamsini…”

“Mtumie anakupima, hata mimi alifanya hivyo…baadaue akanipa pesa…pengine anapima imani yako, wee mpe…utaona…,” alisema Monica, alitunga uongo.Mzee wake hakuwa na pesa nyingi na kweli alikuwa na shida na hiyo elfu hamsini.

“Nishamtumia mbona…”

“Basi, subiri kama sio leo atakupa pesa kesho…anaweza pia kunituma nikuletee…”

“Mmh! Sawa, hebu tuone kama ni kweli…”

**

Monica alioga peke yake bafuni kisha akatoka na kuvaa bikini yake. Alipanga kwenda kwa baba yake kuzungumza naye aweze kumtoa hofu mumewe, ghafla aliona simu yake ikiita maana haikuwa na sauti, akaipokea.

“Haloo sweetie….unaendelea?” Ilikuwa sauti ya kukwaruza ya mzee Mombasa.

“Naendelea vizuri ila nimechoka, jana umenipa shughuli pevu…vipi wewe?”

“Nimekumisi, Monica sijawahi kupewa penzi tamu kama hilo la jana, naomba nikupe zawadi…”

“Zawadi gani mpenzi?”

“Ni surprise…njoo Posta town…”

“Sasa hivi?”

“Ndiyooo….,” alijibu mzee Mombasa.

“Sawa…nakuja mpenzi…,” Monica hakutaka kupoteza muda, alijipodoa kweli kweli na kuvaa ile nguo yake ya kuvutia ambayo siku hii iliacha paja zake wazi kweli kweli. Katika mkoba wake, alihifadhi gauni la heshima, hili alipanga kulivaa wakati wa kwenda kuonana na wazazi wake.

“Dereva anakuja kunichukua mpenzi wangu?”

“Ndiyo, namwagiza sasa hivi…,” alisema Mzee Mombasa.

Seki kama kawaida alipigiwa simu aweze kwenda kumchukua Monica kwa ajili ya kumleta Posta, hiki ni kitu ambacho hakika hakutaka, hivyo alilazimika kumpigia Sakala.

“Vipi, upo kazini kwako? Nataka nije nikupe gari ukamchukue yule demu wa jana wa bosi…”

“Ahaaa, nina kazi lakini kwasababu kuna ujira wangu, njoo fasta…,” Sakala aliwaachia kazi mafundi wadogo, akaenda kuoga bafu za palepale ubungo. Kutokana na demu mwenyewe kuwa mzuri, alilazimika kukodi bodaboda na kununua nguo mpya, hakutaka kuonekana mchafu, alipenda sana Monica. Alivaa fresh na kumsubiri Seki ambaye alifika muda huo huo.

“Sasa sikiliza jamaa yangu, yule demu nenda kamchukue…usimwambie kuwa nimekuagiza mimi, wala usithubutu kuonesha kuwa mtu anaitwa Seki…”

“Kwanini?”

“Sitaki tu, yule demu ni mke wa kaka yangu…”

“Aiseee, ndiyo maana hutaki kuonana naye wala kusikia story zake?”

“Ndiyo, naogopa sana…”

“Sawa nimekuelewa…wanawake hatari sana….,” Sakala alisema akiingia garini na kuongozana na Seki, alipofika nje ya kituo cha mabasi Ubungo, Seki alishuka.

“Mpeleke Posta, jirani na jengo la Mkapa…nitakupa maelekezo…” alisema Seki, wakati huu Sakala alijiuliza ni sababu gani inamfanya mke wa mtu adange namna hiyo? Inawezekana kaka yake Seki, hawezi kumtoa joto na machozi ya mapenzi au ni njaa na tamaa tu za mwanamke zinamsumbua?

**

Monica alivaa kimini ambacho kwa heshima yake kama mke wa mtu, alilazimika kujifunga kanga ili kuficha kimini hicho.Manukato yake yalinukia kila alipopita, majirani walishangaa kwa jinsi Monica alivyoanza kuchukuliwa na gari la kifahari. Wanawake wa mtaani wambea walimsindikiza kwa macho na kumuona akipanda gari la kifahari.Aliduwaah!.

Alipoingia tu, kama kawaida alibadilisha harufu ndani ya gari, manukato yake yakatawala. Aliketi siti ya kushoto mwa dereva, akamsogelea Sakala na kuikamata shingo yakwe kisha akaivuta na kumkumbatia akiendelea na kushusha mvua ya mabusu, akimpigapiga Sakala mgongoni.

“Monica, unanichanganya…kitendo cha kunikumbatia mapigo yangu ya moyo yanaenda kasi…”

“Ahsante, wee mwanaume rijali…najua…”

“Ndiyo, natamani unichunuku…mwili wako mlaini sana Monica…”

“Weee umegusa kifuani.Je, kule kwingine si ndio utapagawa…lainiiii….”

“Samahani, naomba niwe mpenzi wako wa siri?”

“Natembea na bosi wako Saka, ila nitakupa siku moja tu…tena nitakutafuta mwenyewe…” Alisema Monica na kuzidi kumchanganya Saka, alitamani kuambiwa waende muda huo. Ghafla Monica akakumbuka hakumwaga mumewe kuwa anatoka, hivyo alimpigia simu.

“Mume wangu kipenzi, nimepigiwa simu na baba amedai niende…ana mazungumzo nami….” Monica alisema hivyo akiamini mumewe hawezi kumpigia baba mkwe wake.

“Ahaa, kuna tatizo?”

“Hapana, nadhani ni mazungumzo ya kifamilia…”

“Sawa…wasalimie wote…” Kapesa hakuwa na wasiwasi na mkewe, alimwamini sana na wala hakuwaza mkewe angeweza kuwa na mwanaume mwingine kwa jinsi anavyomjali kwa kila kitu.

Je, nini kitaendelea? Usikose simulizi hii siku ya kesho

Leave A Reply