The House of Favourite Newspapers

VAR Yasababisha Balaa Brazil

0

Chama cha Soka nchini Brazil kimesema kitachukua hatua kali kwa Klabu ya Gremio kufuatia vurugu zilizozuka kwenye mchezo wa Ligi Kuu nchini humo siku ya Jumapili, Oktoba 31, 2021.

.

Mashabiki wa Gremio walivamia uwanja na kufanya vurugu kufuatia kipigo cha 3-1 nyumbani dhidi ya Palmeiras.

Mashabiki hao walijaribu kuharibu Mfumo wa VAR uliotumika kulikataa bao lililofungwa ambalo lingefanya ubao kusomeka 2-2 kabla ya kuongezwa bao la 3.

Matokeo hayo ya kipigo yameifanya klabu hiyo kusalia katika eneo la timu zitakazoporomoka daraja kwenye msimamo wa ligi kuu nchini Brazil.

Leave A Reply