KAMPUNI ya Mawasiliano ya Simu ya Vodacom leo imekabidhi msaada wa kompyuta 10 katika Kituo cha Child In The Sun cha Mbezi Makabe jijini Dar es Salaam kwa watoto wanaoelelewa kituoni hapo. Msaada uliotolewa na Vodacom Tanzania Foundation kwa ajili ya mafunzo yao kituoni hapo.