Vodacom Yakabidhi Bima za Afya 200 Kwa Wanawake na Watoto Jijini Mwanza
Kampuni ya simu za mikononi ya Vodacom, imetoa bima za afya 200 kwa wanawake na watoto 200 pamoja na zawadi mbalimbali kupitia Kampeni ya Sambaza Shangwe, Gusa Maisha jijini Mwanza.
Kupitia kampeni hii wateja wanayo fursa ya kushinda zawadi mbalimbali ikiwemo bodaboda, luninga, simu za mkononi, router za 4G na 5G pamoja na pesa taslimu kila wiki kuanzia shilingi laki tano mpaka milioni 10 kwa kununua vifurushi, kufanya malipo kwa M-Pesa na kupakua DJ Mixes kupitia Mdundo.