Kampuni ya Mawasiliano Vodacom imeshinda Tuzo ya Kampuni Bora ya Mawasiliano kwenye maonesho ya sabasaba jijini Dar es Salaam. Vodacom Tanzania ilishinda tuzo hiyo baada ya kuwa kinara kutokana na huduma bora zilizotolewa na kampuni hiyo kwenye maonesho ya 45 ya biashara ya kimataifa kupitia kundi la sekta ya mawasiliano.