The House of Favourite Newspapers

FT: Yanga 0-1 Mbao FC, Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza

0

FULL TIME

Mbao wanaibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Yanga, wanashangilia kwa nguvu kwa kuwa wanajihakikishia kubaki katika Ligi Kuu ya Vodacom.

Dakika ya 96: Mchezo umemalizika, mwamuzi anapuliza kipenga cha kukamilisha kipindi cha pili.

Dakika ya 86: Simba wanapata kona, wanaanzisha kona fupi lakini inakosa faida.

Dakika ya 85: Yanga wanafanya mabadiliko, anatoka Haruna Niyonzima anaingia Matheo.

Dakika ya 84: Yanga wanapongeza presha, wanalishambulia lango la Mbao lakini wanakosa nafasi wanazopata.

Dakika ya 80: Beki Juma Abdul wa Yanga anapewa kadi ya njani kwa kumchezo mbaya.

Mwamuzi anampa kadi ya njano Simon Msuva kwa kumparamia na kusababishaguke chini.

Dakika ya 77 Kunatgokea purukushani uwanjani, wachezaji wa Yanga wanamvaa mwamuzi.

Dakika ya 71: Yanga wanapata kona, inapigwa lakini walinzi wanaumiliki, kipa wa Mbao anauwahi mpira na kuudaka.

Dakika ya 69: Yanga wanapata kona, inapigwa lakini Mbao wanaondoa mpira.

Mbao wanafanya mabadiliko, wanamtoa Habib Haji ambaye ni mfungaji wa bao lao , anaingia Rajish Kotecha.

Dakika ya 65: Yanga wanapata nafasi, Emmanuel Martine anabaki yeye na kipa lakini kipa wa Mbao anafanya kazi nzuri.

Dakika ya 64: Inapigwa kona kunatokea vuta nikuvute lakini mpira unaokolewa, inakuwa kona nyingine. Mchezo ni mkali hasa.

Dakika ya 63: Chirwa anachezewa faulo karibu na lango la Mbao, inapigwa faulo, mpira unatoka inakuwa kona.

Dakika ya 53: Kunatokea mvutano kati ya wachezaji wa Mbao na Yanga. Mzozo ni mkubwa na mchezo umesimama.

Dakika ya 50: Simba wameanza kipindi hiki lakini kasi yao siyo kubwa kama ilivyokuwa awali.

Mwamuzi anaanzisha kipindi cha pili.

Kipindi cha pili kimeanza.

Tujikumbushe Kikosi Cha Yanga kilichoanza katika mchezo wa leo:

1.Beno Kakolanya 2.Juma Abdul 3.Oscar Joshua 4.Nadri Haroub 5.Vicent Bosou 6.Thaban Kamsoko 7.Simon Msuva 8.Justine Zulu 9.Obrey Chirwa 10.Haruna Niyonzima 11.Geofrey Mwashuya

Tujikumbushe Kikosi Cha Mbao FC kilichoanza katika mchezo wa leo

1.Benedict Haule 2.David Mwassa 3.Asante Kwasi 4.Yusuph Ndikumana 5.Salmin Hoza 6.Jamal Mwambeleko 7. Ibrahim Njohole 8.Pius Buswita 9.George Sangija 10.Boniface Maganga 11.Habibu Haji

 

Dakika ya 45: Mwamuzi wa akiba anaonyesha dakika 2 za nyongeza.

Dakika ya 43: Mbao wanatoa upinzani mkali kwa Yanga, wanapata kona mbili mfululizo, lakini mabeki wa Yanga wanakuwa makini na kuondoa hatari.

Dakika ya 39: Yanga wanajibu mapigo, Msuva anapata nafasi lakini kipa anakuwa makini na kuudaka mpira huo.

Dakika ya 39: Yanga wanajibu mapigo, Msuva anapata nafasi lakini kipa anakuwa makini na kuudaka mpira huo.

Dakika ya 37: Mbao wanafanya shambulizi kali, linapigwa shuti linatoka nje kidogo ya lango.

Dakika ya 35: Yanga wanafika langoni, Juma Abdul anapanda kusaidia mashambulizi upande wa kulia.

Dakika ya 30: Yanga wanafika kwenye lango la Mbao mara kadhaa lakini walinzi wa Mbao wanakuwa makini na kuondoa. Shangwe ni nyingi kutoka kwa mashabiki hapa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, mitaa ya Kirumba.

Kikosi cha timu ya Yanga

Dakika ya 28: Kasi ya mchezo imekuwa kubwa zaidi, Yanga wanapambana kutafuta bao la kusawazisha.

Dakika ya 30: Yanga wanafika kwenye lango la Mbao mara kadhaa lakini walinzi wa Mbao wanakuwa makini na kuondoa. Shangwe ni nyingi kutoka kwa mashabiki hapa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, mitaa ya Kirumba.

Dakika ya 28: Kasi ya mchezo imekuwa kubwa zaidi, Yanga wanapambana kutafuta bao la kusawazisha.

Dakika ya 23: Habib Haji anaipatia Mbao bao la kwanza, amefanya kazi nzuri ya kuwatoka walinzi wa Yanga na kupiga shuti kali lililojaa wavuni. Mbao wanaongoza bao 1-0.

Dakika ya 23: Habib Haji anaipatia Mbao bao la kwanza, amefanya kazi nzuri ya kuwatoka walinzi wa Yanga na kupiga shuti kali lililojaa wavuni. Mbao wanaongoza bao 1-0.

GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO

Dakika ya 18: Mpambano ni mkali na una kasi kubwa, Chirwa wa Yanga alipata nafasi ya kukimbia na mpira na kulikaribia lango lakini mpira ukatoka nje.

Dakika ya 14: Kona inapigwa lakini walinzi wa Yanga wanaondoa hatari.

Dakika ya 13: Mbao wanapata kona, lakini kunatokea mvutano baina ya wachezaji wa Mbao na wa Yanga, mwamuzi anazungumza nao na mchezo unaendelea.

Dakika ya 10: Mashabiki ni wengi na kasi ya mchezo inaongezeka.

Dakika ya 5: Mbao wanaendeleza kasi, kipa wa Yanga Beno Kakolanya anakuwa na kazi ya ziada kuwapanga walinzi wake.

Dakika ya 2: Mbao wanafika kwenye lango la Yanga na kufanya shambulizi kali lakini walinzi wa Yanga wanakuwa makini wanaokoa.

Dakika yua 1: Mchezo umeanza kwa kasi.

Mwamuzi anaaznisha mchezo

Leave A Reply