The House of Favourite Newspapers

Vyuo Vikuu 10 Bora Zaidi Barani Afrika

1  University of Cape Town – Cape Town, South Africa

Image result for university of cape town south africa

The University of Cape Town (UCT), kiko katika miteremko ya mlima uitwao Devil’s Peak jijini  Cape Town, kikiwa ndicho chuo kikuu kikongwe zaidi nchini Afrika Kusini.  Kilianzishwa mwaka 1829 na kina wanafunzi zaidi ya 25,000 walimu wapatao 1,000.

2  American University in Cairo – Cairo, Egypt

Image result for american university in cairo

 

Kilianzishwa mwaka 1919 huchukua wanafunzi wapatao 16,000 kila mwaka.

Miongoni mwa wahitimu wake maarufu ni waziri wa zamani wa ulinzi wa Japan, Yuriko Koike, mwanadiplomasia na mwandishi wa habari wa Romania, Dan Stoenescu, na mtayarisha filamu wa kwanza wa kike wa Saudi Arabia, Haifa Al-Mansour.

3  Al Akhawayn University – Ifrane, Morocco

Kilianzishwa mwaka 1995 kikiwa kimejengwa katika eneo la Milima ya Atlas.

4  University of Nairobi – Nairobi, Kenya

Kilianzishwa 1956 ambapo pamoja na kuchukua wanafunzi wapatao 70,000, kina walimu wapatao 1,600 na huchukua wastani wa wanafunzi 120 kutoka nchi za nje kila mwaka.

5  Makerere University – Kampala, Uganda

Image result for makerere university

 

Kilianzishwa 1922 na huchukua wanafunzi zaidi ya 40,000 kila mwaka.  Ni chuo kikuu kikongwe zaidi nchini Uganda.

University of Ghana at Legon – Accra, Ghana

Image result for University of Ghana at Legon

Kikiwa kilianzishwa kama tawi la University of London, baadaye kikajitegemea mwaka.  Huchukua wanafunzi zaidi ya 38,000 kila mwaka.

7  University of Ibadan – Ibadan, Nigeria

Image result for University of Ibadan

Kilianzishwa 1948, kiko pembeni mwa jiji la Ibadan.  Kinajulikana pia kama Unibadan au UI. 

8  University of Botswana – Gaborone, Botswana

Kilianzishwa 1982, kikiwa na makazi matatu ya wanafunzi (campuses) katika jiji la  Gaborone, Francistown na Maun. Huchukua wanafunzi karibu 19,000 kwa mwaka.

9  University of Dar es Salaam – Dar es Salaam, Tanzania

Image result for University of Dar Es Salaam

Kilianzishwa 1961 kama tawi la  University of London baadaye kikawa mshiriki wa University of East Africa (UEA) mwaka 1963 baada ya Tanganyika kupata uhuru kutoka kwa Uingereza.  Mwaka 1970 UEA ikagawanyika na kuanzisha vyuo vikuu vitatu vyenye kujitegemea vya   Makerere University cha Uganda, University of Nairobi cha Kenya, na University of Dar es Salaam.

10  Addis Ababa University – Addis Ababa, Ethiopia

Addis Ababa University (AAU) kilianzishwa 1950 kama University College of Addis Ababa (UCAA) kikiwa na wanafunzi 33 ambapo sasa kina wanafunzi 48,673.

Tangu kuanza kwake, wanafunzi zaidi ya 222,000 wamehitimu hapo.

 

Comments are closed.