The House of Favourite Newspapers

Wafanyakazi wa DCB washerehekea kumaliza salama zoezi la uuzaji hisa

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya  DCB, Godfrey Ndalahwa (wa tatu kulia), akigonga glasi na baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo kushereheka kumaliza salama msimu wa uuzaji wa hisa za benki hiyo uliyoanza Novemba 12 mwaka jana na kuhitimishwa Januari 31 mwaka huu. Hisa moja iliuzwa kwa bei pungufu ya shs 265. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi.
Mkurugenzi wa Mikopo wa Benki ya Biashara ya DCB, Isidory Msaki (kushoto), akifungua ‘Shampaigne’ huku baadhi ya maofisa wa benki hiyo wakishangilia katika hafla ya wafanyakazi hao kusherehekea kumaliza salama msimu wa uuzaji wa hisa za benki hiyo uliyoanza Novemba 12 mwaka jana na kuhitimishwa Januari 31 mwaka huu. Hisa moja iliuzwa kwa bei pungufu ya shs 265. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji, Godfrey Ndalahwa, Mkurugenzi wa Fedha, Zacharia Kapama na wafanyakazi wengine.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya  DCB, Godfrey Ndalahwa ( kulia), akigongesha glasi na Meneja wa Tawi la Magomeni, Haika Machaku (kushoto),  kushereheka kumaliza salama msimu wa uuzaji wa hisa za benki hiyo uliyoanza Novemba 12 mwaka jana na kuhitimishwa Januari 31 mwaka huu. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Godfrey Ndalahwa (katikati), akishangilia wakati baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo wakifungua chupa za ‘champagne’ katika hafla ya wafanyakazi hao kusherehekea kumaliza salama msimu wa uuzaji wa hisa za benki hiyo uliyoanza Novemba 12 mwaka jana hadi Januari 31 mwaka huu. Hisa moja iliuzwa kwa bei pungufu ya shs 265. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi.
Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya DCB, wakiwa na nyuso zenye furaha na matumaini  katika hafla hiyo. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB, Godfrey Ndalahwa (kulia), akigonganisha glasi pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa DCB katika hafla hiyo.

 

Comments are closed.