The House of Favourite Newspapers

WAJAPANI WAMJIA JUU KIM KARDASHIAN NA BIDHAA ZAKE ZA NGUO ZA NDANI

MWANAMITINDO maarufu Duniani Kim Kardashian amejikuta akiingia matatani na Wajapan baada ya kuzindua bidhaa zake za nguo za ndani na kuziita jina la ‘Kimono’ na kuelezwa kuwa jina hilo ni vazi ambalo lina heshima kubwa nchini Japan.

Kimono ni vazi ambalo huvaliwa maeneo maalum kwa Japan na hivyo kutumika kama jina la nguo za ndani ni ukosefu wa heshima kwa nguo hizo hivyo Kim Kardashian ameamua kubadilisha jina hilo kutokana na Wajapan kumuwashia moto.

Image result for kimono dress of japan

Mwanamitindo uyo alienda mbali na kuomba radhi kupitia ukurasa wake wa instagram na kusema akuwa atabadilisha jina la nguo zake mpya.

Comments are closed.