Wakazi wa Jiji la Dar walivyofurahia Ushindi wa Dk Magufuli
Baadhi ya wakazi wa Jiji la Dar wakiwa katika Mitaa ya Kisutu wakifurahia ushindi wa Dk. Magufuri, baada ya kukabidhiwa cheti cha ushindi kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mh. Jaji Damian Lubuva.
Mmoja wa kina mama akishikilia khanga yenye ujumbe wa ushindi.
Hamasa za ushindi wa Dk. Magufuli katika baadhi ya mitaa zikiwa zimetawaliwa na maandamano ya furaha.
Hekaheka za furaha zikiendelea baadhi ya mitaa ya Jiji la Dar za kusherehekea ushindi wa Dk. Magufuli.
WAKAZI wa Jiji la Dar es Salaam na viunga vyake, leo Ijumaa walikuwa na shamrashamra za kusherehekea ushindi wa Rais Mteule wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli aliyeshinda kwenye kinyang’anyiro cha uchaguzi kilichofanyika Oktoba 25, mwaka huu.
Na DENIS MTIMA/GPL