Dully Sykes.
WAKONGWE kwa zaidi ya miaka kumi kunako Muziki wa Bongo Fleva, Dully Sykes, Inspector Haroun, Nature na wengine kibao, Mei 28, mwaka huu wanatarajiwa kulitikisa jukwaa la Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live uliopo Mbagala-Zakhem jijini Dar.
Juma Nature
Akichonga na Showbiz, Meneja wa Dar Live, Juma Mbizo alisema kuwa mbali na wakali hao, wengine watakaoliteka jukwaa ni Afande Sele, Jafarai, Sister P, Suma G, Abby Skillz na wengineo.
“Hii ni moja ya shoo za kibabe kuwahi kutokea Dar Live pekee. Ambapo niwaambie tu tutakuwa na makundi kibao ya wakongwe ambayo ni Joint Mob, Zig Zag Crew, Solid Ground Family, Mabaga Fresh, Manzese Crew na mengineyo,” alisema Mbizo na kumalizia kuwa kiingilio kitakuwa 7,000 tu getini.
KUNUNUA NA KUSOMA MAGAZETI YA GLOBAL PUBLISHERS ONLINE, INGIA HAPA==>VODACOM M-PAPER APP
*********
JIUNGE NA SOCIAL MEDIA ZETU
KWA HABARI ZA KITAIFA, KIMATAIFA, MASTAA NA MIKASA YA KUSISIMUA
INSTAGRAM: @Globalpublishers
ERIC SHIGONGO INSTAGRAM: @ericshigongo
TWITTER: @GlobalHabari
FACEBOOK: @GlobalPublishers
SUBSCRIBE YOU TUBE: Global TV Online
GLOBAL TV ONLINE: www.globaltvtz.com
HADITHI ZA KUSISIMUA NA MBINU ZA UJASIRIAMALI, ERIC SHIGONGO FACEBOOK PAGE:@shigongotz