The House of Favourite Newspapers

WANACHUO WALIOTENGENEZA MITA YA MAJI WATUA GLOBAL

Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha St. Joseph cha jijini Dar es Salaam wakiwa na mita yao ya maji nje ya ofisi za Global Group zilizopo Sinza-Mori jijini  Julai 19, 2019. Kutoka kushoto ni Mwalimu wa Chuo hicho, Ruben Jonson, akiwa na wanafunzi wake Khadija Mustapha (wa pili kutoka kushoto),  Edina Pesha  na Hashim Shukuru.

 

WANAFUNZI wa Chuo Kikuu cha St. Joseph cha jijini Dar es Salaam waliobuni mita ya kisasa na mfumo wa kulipia bili ya maji inayofanya kazi kwa mfumo kama wa LUKU na inatumia umeme wa jua, Ijumaa, Julai 19, 2019, wamefanya ziara ofisi za Global Group zilizopo Sinza-Mori jijini Dar  wakiambatana na mwalimu wao kuonyesha uvumbuzi wao ambao unaenda kutatua changamoto za malipo ya huduma ya maji nchini.

Edina Pesha akizungumzia  changamoto za malipo ya huduma ya maji nchini wanayokutana nazo wateja wakati wa mahojiano na +255 Global Radio.

Mita hiyo imetengenezwa na Khadija Mustapha,  Edina Pesha na Hashim Shukuru  kwa muda wa wa miezi minane  na wametumia kiasi cha Tsh. 900,000/- kwa kununua baadhi ya vifaa kama mabomba ya maji,  Micro controller, Solar Panel, Valve, mbao,  n.k

 

Wakiongea na +255 Global Radio wamesema wanaendelea kuboresha mfumo huo ili kuwasadia watumiaji wa maji nchini na wanatarajia wateja wao kuwa taasisi za serikali na watu binafsi.

Wanachuo hao wakiwa katika mahojiano maalum katika studio ya Global Radio.

Kwa mujibu wa wanachuo hao, mteja atakayatumia mita hiyo atakuwa akilipia bili kupitia simu yake ya mkononi na hakuna mteja atakayeweza  kutumia maji bila kulipia na kwamba wateja wakaojaribu kuwaibia kupitia mita hiyo watatumiwa ujkumbe maalum wa kuwajulisha mita namba ambayo inataka kufanya uhalifu huo.

…Wakiwa katika picha na Meneja wa +255 Global Redio, Bori Mbaraka (katikati) baada ya mahojiano.

Pamoja na uvumbuzi huo, wanatarajia kutafuta  mfadhili wa kuwawezesha  kutengeneza mita hizo na kuzisambaza kwenye jamii  na kufungua kiwanda kwa ajili ya kubuni vitu mbalimbali vitakavyowawezeha Watanzania kutatua changamoto zao.

Mhariri Mtendaji wa Global Publishers, Saleh Ally (wa pili kutoka kushoto) akiwa na wanachuo hao. 
Mhariri wa Championi Jumatatu, Ezekieli Kitula (mwenye shati la draft) akiongea jambo.
… Wakisani kitabu cha wageni.
…Muonekano wa mita hiyo

PICHA NA GLOBAL RADIO

Comments are closed.