Wanahabari Mwanza Wapigwa Msasa Utoaji wa Habari
WIZARA ya afya kwa kushilikiana na Mradi wa USAID Tulonge Afya fhi 360 wametoa mafunzo kwa wanahabari jijini Mwanza juu ya utoaji habari wakati wa maandalizi ya uzinduzi wa Majukwaa mawili ya mawasiliano ya afya kwa watu wazima litakaloitwa “NAWEZA” na kwa vijana “SITETELEKI” ili kufikisha elimu sahihi itakayoijengea jamii ya Watanzania uwezo na kubadilisha mitizamo na tabia zao za kiafya na kuleta matokeo chanya.
Mafunzo hayo yalifanyika jijini Mwanza mwishoni mwa wiki katika Hotel ya Gold Crest ambapo yalipata mwitikio mkubwa na ulewa mzuri kwa wanahabari waishio jijini Mwanza.
Mafunzo hayo yaliendeshwa na wataalamu mambo ya Afya kutoka Wizara ya Afya na USAID Tulonge Afya fhi 360.
NAWEZA ni jukwaa litakalolenga kuwafikia wananchi tofauti tofauti itachangia kuboresha afya na ustawi wa Watanania wengi, itakuwa ikibadilika badilika ili kukidhi mahitaji ya maeneo mengine ya kiafya muhimu kwa walengwa hao ama makundi mengine hususani watu wazima.
SITETELEKI ni jukwaa litakalolenga zaidi kuwafikia Vijana wenye umri kati ya 15 – 24, wanaokabiliwa na changamoto nyingi za malengo ya maisha.
Na Mwandishi wetu – Mwanza
Comments are closed.