The House of Favourite Newspapers

Wananchi wa Buchosa Washiriki Misa Ya Kuwaombea Wazazi wa Mhe. Shigongo

0
Mke wa Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Buchosa, Bi Veneranda Shigongo (kushoto) na dada yake wakifuatilia ibada fupi ya kuwaombea wapendwa wao waliotangulia mbele za haki.
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Bupanwa na vijiji vya jirani wakiwa katika ibada fupi ya kuwaombea wapendwa waliotangulia mbele za haki nyumbani kwa Mbunge Eric Shigongo.
Mbunge wa Jimbo la Buchosa Mhe. Eric Shigongo (kulia) akifuatilia ibada fupi iliyokuwa ikiendelea.
Wanafamilia ya Eric Shigongo wakiwa katika ibada fupi ya kuwaombea wapendwa wao.
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Bupanwa na vijiji vya jirani wakiwa katika ibada fupi ya kuwaombea wapendwa waliotangulia mbele za haki nyumbani kwa Mbunge Eric Shigongo.
Sehemu ya Madiwani wa jimbo la Buchosa walipoandaliwa wakifuatilia kilichokuwa kikiendelea.
Baba mdogo wa Mhe. Eric Shigongo aitwaye Mzee Zabron ( kulia) akishiriki ibada fupi ya kuwaombea wapendwa wao waliotangulia mbele za haki.
Ndugu na jamaa wakishiriki ibada fupi nyumbani kwa Mbunge Shigongo.
Mwanakijiji wa Mwangika aitwaye, Vitus Francis (kulia) akiwa ni mmoja wa walioshiriki ibada fupi ya kuwaombea waliotangulia mbele za haki nyumbani kwa Mbunge Mhe. Eric Shigongo.
Ibada ikiendelea.
Baadhi ya wanakwaya wa Bupandwa wakiimba nyimbo.
Paroko wa Kanisa Katoliki Mwangika Parokia ya Mt. Yakobo Mkuu, Padri Hilary Faraja akiendesha misa fupi  Bupandwa Mhela ya kuwakumbuka wazazi wa Eric Shigongo na ndugu wengine walio mbele za haki.
Paroko wa Kanisa Katoliki Mwangika Parokia ya Mt. Yakobo Mkuu, Padri Hilary Faraja akiendesha misa fupi  Bupandwa Mhela ya kuwakumbuka wazazi wa Eric Shigongo na ndugu wengine walio mbele za haki.
Kutoka kushoto ni Diwani wa kata ya Luharanyonga Mchungaji Samike, Mbunge wa Jimbo la Buchosa, Eric Shigongo, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM ) Wilaya ya Sengerema, Augustine Makoye, Katibu wa CCM Wilaya ya Sengerema Muksini Zikatimu (mwenye shati la drafti).
Kutoka kushoto ni Diwani wa kata ya Luharanyonga Mchungaji Samike, Mbunge wa Jimbo la Buchosa, Eric Shigongo, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM ) Wilaya ya Sengerema, Augustine Makoye, Katibu wa CCM Wilaya ya Sengerema Muksini Zikatimu na Mjumbe wa Kamati Kuu Wilaya ya Sengerema, David Akida Bwana.
Askari wa Jeshi la Polisi kutoka kituo cha Polisi cha Bupandwamhella wakiwa wameungana na wanakijiji na majirani wa kijiji hicho nyumbani wa Mbunge Mhe. Eric Shigongo.
Askari Polisi wa Kituo cha Bupandwa wakifuatilia kwa makini kilichokuwa kikiendelea katika misa hiyo fupi.
Mbunge wa Jimbo la Buchosa Mhe. Eric Shigongo akitoa neno la shukrani kwa wageni waalikwa na ndugu na jamaa kwa kufika kuungana na wanafamilia.
Mbunge wa Jimbo la Buchosa Mhe. Eric Shigongo akitoa neno la shukrani kwa wageni waalikwa na ndugu na jamaa kwa kufika kuungana na wanafamilia.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM ) Wilaya ya Sengerema, Augustine Makoye akitoa salamu za chama Cha Mapinduzi kwa familia ya Mzee Bukumbi.
Mtoto wa Mhe.Mbunge wa Jimbo la Buchosa aitwaye, Tanzania Shigongo akisikiliza kwa makini misa iliyokuwa ikiendelea.
Mtoto Baraka Shigongo (katikati) akisikiliza kwa makini misa iliyokuwa ikiendelea.
Paroko wa Kanisa Katoliki Mwangika Parokia ya Mt. Yakobo Mkuu, Padri Hilary Faraja akibariki makaburi ya wazazi wake Shigongo.
Mbunge wa Jimbo la Buchosa Mhe. Eric Shigongo na Paroko wa Kanisa Katoliki Mwangika Parokia ya Mt. Yakobo Mkuu, Padri Hilary Faraja (katikati) wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali.

 

Wakati sikuku ya Krismasi ikiwa imemalizika Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Global Group na Mbunge wa Jimbo la Buchosa Mhe. Eric Shigongo amesherehekea sikukuu hiyo kwa kufanya Misa fupi ya kuwakumbuka wapendwa wake waliotangalia mbele za haki akiwemo baba yake mzazi Marehemu, James Bukumbi na Bi. Asteria Kapela ambao wote wapo mbele za haki.

 

Akiendesha ibada fupi Paroko wa Kanisa Katoliki Mwangika Parokia ya Mt. Yakobo Mkuu, Padri Hilary Faraja amewataka wakazi wa Bupandwa na vitongoji vingine vilivyoungana katika misa hiyo kutenda matendo mema yenye kuumpendeza mungu katika kipindi hiki cha kusherehekea sikukuu ya Krismasi na Mwaka mpya.

 

Amesema kuwa mwanadamu anapaswa kufanya yale yote yanayompendeza Mungu, kuoneshaa upendo kwa ndugu jamaa na marafiki, kusaidia familia zisizojiweza kwa kutoa msaada.

Pia Paroko huyo amewataka viongozi walio katika nyadhifa mbalimbali kuenenda na nyakati ambapo kwa sasa dunia inaenda katika digitali na hivyo kutumia fursa hiyo kuonesha yale wanayoyafanya katika maeneo yao kupitia mitandao mbalimbali ili jamii iweze kuyaona.

 

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Buchosa Mhe. Eric Shigongo amewashukuru wananchi wote waliofika kuungana na wanafamilia ya Bukumbi na kwamba wanawapenda sana na kama familia itaendelea kushirikiana katika shughuli zote za kijamii na kifamilia ili kuendeleza umoja waliouacha wazazi wao ambao siku ya leo wanakumbukwa kwa kuwaombea.

 

Leave A Reply