The House of Favourite Newspapers

Wasanii Walivyojipanga Kuadhimisha Siku Ya Kimataifa Ya Kuigiza Jukwaani

0
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini, Dk. Kiagho Kilonzo alivyokuwa akizungumzia maadhimisho hayo leo.

Dar es Salaam 27 Machi 2024: Ikiwa leo Macho 27 ni Siku ya Kimataifa ya Maonesho ya Sanaa ya Kuigiza jukwaani na filamu Wadau wa sanaa nchini kwa kushirikiana na Bodi ya Filamu wameelezea jinsi walivyojipanga kuadhimisha Siku ya Kimataifa kwa progam maalum iitwayo TAMBA NA JUKWAA.

Dk Kilonzo akizungumzia maadhimisho hayo, kulia ni msanii mkongwe wa Bongo Muvi, Lumole Mutovolwa maarufu Big anayemfuatia ni mkali wa maigizo ya jukwaani na mashairi ya kughani, Mgunga Mwamnyenyerwa na kushoto ni Mwalimu wa sanaa ya maigizo kutoka Kanisa la KKKT Usharika wa Ubungo, Martin Mung’ong’o.

Akizungumza na wanahabari leo, Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini, Dk. Kiagho Kilonzo amesema bodi hiyo ambayo jukumu lake siyo filamu peke yake isipokuwa mpaka maonesho ya jukwaani mwaka huu wamejipanga kuadhimisha siku hiyo kwa matukio kadhaa yatakayokwenda na program iitwayo Tamba na Jukwaa.

Mwalimu wa sanaa ya maigizo kutoka Kanisa la KKKT Usharika wa Ubungo, Martin Mung’ong’o akizungumza jinsi walivyojipanga kwenye onesho lao la pasaka.

Dk. Kilonzo amesema program ya TAMBA NA JUKWAA itahusisha maigizo mawili ambapo Machi 29   kutakuwa na igizo la pasaka katika eneo la Kanisa la KKKT Ubungo Dar na kufuatiwa na onesho la Aprili 20 mwaka huu liitwalo JUKWAA LA MTAA. litakaloongozwa na Ayubu Kondo Bongwe maarufu kama Black Jesus.

HABARI/PICHA NA RICHARD BUKOS /GPL 

Leave A Reply