Washindi droo ya tatu ‘Shinda Nyumba’ wakabidhiwa zawadi
Mshereheshaji wa hafla hiyo, Chaku Shemungia (kushoto) akimhoji, Charles Chawala, baada ya kukabidhiwa simu ya kisasa (smart phone) aliyojishindia kwenye mchezo huo.
Happyness Kimaro akimchukulia zawadi ya seti ya vyombo vya chakula (dinner set) Asha Mussa aliyemtuma baada ya kutingwa na majukumu.
Isaac Wilyadi akipokea zawadi ya king’amuzi cha TING.
Magreth Chacha alishinda na kupewa king’amuzi cha TING.
Pendo Mkanda akipokea king’amuzi cha TING.
Zalika Ally wa Lushoto mkoani Tanga akipokea televisheni-bapa na king’amuzi cha TING kutoka kwa Mhariri wa Championi Jumamosi, Elius Kambili.
Washindi wakiwa kwenye picha ya pamoja.
WASHINDI wa droo ya tatu ya bahati nasibu ya Shinda Nyumba inayoendeshwa na kampuni ya Global Publishers watoaji wa magazeti ya Uwazi, Ijumaa, Amani, Risasi, Ijumaa Wikienda na Championi, leo wamekabidhiwa zawadi zao kwenye hafla iliyofanyika ofisi hizo zilizopo Bamaga- Mwenge jijini Dar. Droo hiyo ilichezeshwa mwishoni mwa wiki iliyopita katika viwanja vya Bakhresa vilivyopo Manzese jijini.
HABARI/PICHA NA RICHARD BUKOS / GPL