Ikiwa ni Jumatano ya Aprili 22, 2020, timu ya maofisa masoko ya Global Publishershers imeendelea na kulisambaza gazeti la Betika ambalo ni mahususi kwa masuala ya kubeti ambapo leo wasomaji wa maeneo ya Lumo, Machimbo na maeneo mengine ya jiji la Dar es Salaam wamejipatia gazeti hilo.
Betika hutolewa bure kwa watu wenye umri kuanzia miaka 18, linachapishwa na Kampuni ya Global Publishers na huingia mtaani kila siku za Jumatano.
Gazeti hilo lenye kurasa 20 za rangi linalojihusisha na masuala ya betting na lotto, lina takwimu za ligi tofauti na matangazo mbalimbali ya biashara.
Baadhi ya wasomaji waliokutana na timu ya maofisa masoko ya Global Publishers, wa maeneo ya Rumo, Machimbo wamezidi kulisifia gazeti hilo kwa kuwa mkombozi waokutokana na kurahisisha kwenye masuala ya michezo ya kubeti.
Gazeti hilo heshima yake imeendelea kukua siku hadi siku na sasa lina watangazaji wengi ambao wanatangaza biashara zao kupitia Betika kwa bei nafuu.
Wote wanaofanya kazi na Betika wanapata ofa ya kutangaziwa biashara zao kwenye mitandao ya kijamii ya Kampuni ya Global Publishers katika Instagram, Facebook, Twitter na Global TV Online.
Ili kuweza kufahamu namna ya kutangaza biashara zako unaweza kufika katika ofisi za Global Group zilizopo Sinza Mori ama kutembelea mitandao yetu ya kijamii ya Global Publishers.