The House of Favourite Newspapers

Watakaopandisha Bei ya Saruji Kunyang’anywa Leseni

0

SERIKALI imesema itawachukulia hatua kali za kisheria, ikiwemo kuwanyang’anya leseni wale wote watakaobainika kuuza saruji kwa bei ya juu.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigella, mara baada ya kutembelea viwanda vya saruji vilivyopo jijini Tanga na kukuta uzalishaji ukiendelea.

Amesema bei ya kiwandani ni kati ya shilingi  10,600 kwa mkoa wa Tanga na nje ya mkoa ni shilingi 11,600 kwa mfuko moja.

Aidha amesema kutokana na kutokuwepo kwa ongezeko la bei kutoka viwandani ya bei ya saruji itabaki kama ilivyokuwa awali na si vinginevyo.

Leave A Reply