Watalii 6 Waliofariki Hifadhi ya Taifa Kenya Wapatikana
WATU sita wameripotiwa kufariki katika Hifadhi ya Kitaifa ya Hell’s Gate nchini Kenya baada ya kusombwa na maji ya mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa siku ya Jumapili, Septemba 1 mwaka huu.
Shirika la wanyamapori nchini Kenya (KWS), limeifungia hifadhi hiyo baada ya tukio hilo liliwasomba watalii sita ambao ni raia wa Kenya na raia mmoja wa kigeni ambaye bado hajulikani alipo na shughuli za kumtafuta zinaendelea, imesema KWS.
Vyombo vya habari nchini Kenya vimeripoti kuwa jana Jumatatu miili hiyo imepatikana.
Hifadhi hiyo inasifika kwa mandhari ya kupendeza ambayo pia imetokea katika filamu ya The Lion King na ya “Tomb Raider: The Cradle of Life” ya mwaka 2003.
Comments are closed.