The House of Favourite Newspapers

Watatu Kati Ya Sita Waliotekwa Na Wasiojulikana, Waonekana

Vijana watatu (kutoka kushoto) waliopotea na kupatikana leo wakinywa chai.
Jinsi walivyokutwa kabla ya kupewa chai. Walikuwa wamefungwa kamba kwa pamoja.

 

WATU watatu kati ya sita waliotoweka katika mazingira ya kutatanisha usiku wa kuamkia Ijumaa,  Aprili 6, 2018 katika Kijiji cha Mitambuuni shehia ya Mtambwe, Mkoa wa Kaskazini Pemba wameonekana alfajiri ya leo Jumapili Aprili 8, 2018  katika Kijiji cha Mkungu Jimbo la Mtambile wilayani Mkoani.

 

Kamanda wa polisi Mkoa wa Kusini Pemba, Sheikhan Mohamed Sheikhan, amethibitisha kupatikana kwa watu  hao ambao ni vijana, kuwa ni Said Shanani Mohamed (16),  Juma Kombo Fimbo (17) na Abdallah Khamis Abdallah (19).

Comments are closed.