Wateja na Mawakala wa Airtel Money Wajishindia Mkwanja na Tesa Kimilionea
KAMPUNI ya Airtel Tanzania leo imechezesha droo ya 11 ya promosheni ya Airtel Money Tesa Kimilionea ambapo wateja 100 wamejishindia Tzs100,000 kila mmoja huku wengine wawili wakijishindia Tzs1,000,000 kwa kila mmoja.
Promosheni ya Tesa Kimilionea ni kwa ajili ya wateja pamoja na wakala wa Airtel na wanaingia kwenye droo ya kujishindia pesa taslimu Tzs100, 000, Tzs1, 000,000 au promosheni kubwa ya Tzs10, 000,000 kila mwisho wa mwezi pale wanapotumia huduma yeyote ya Airtel Money.