The House of Favourite Newspapers

Wateja wa Airtel kupata ofa ya simu bomba kupitia SMARTIFONIKA Bazaar‏

0

imageMeneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando akionyesha simu aina ya Magnus Bravo Z10 iliyo na ofa ya kifurushi cha kuanzia cha bure chenye dakika 150 za kupiga simu, SMS 150 pamoja na kifurushi cha internet chenye ujazo w MB 150 kila mwezi kwa muda wa mienzi 6  katika uzinduzi wa Smartphone Bazaar iliyopo Mlimani City. Pichani ni wafanyakazi wa kitengo cha huduma kwa wateja wa Airtel

image[1]Moja ya wateja waliotembelea Smartphone Baazar Mlimani City akijipatia simu yake aina ya Magnus Bravo Z10 iliyo na ofa ya kifurushi cha kuanzia cha bure chenye dakika 150 za kupiga simu, SMS 150 pamoja na kifurushi cha internet chenye ujazo w MB 150 kila mwezi kwa muda wa mienzi 6 toka kwa watoa huduma wa Airtel Bi Zainab Hamidu. Airtel imezindua Smartphone Bazaar katika msimu huu wa sikukuu ili kuwawezesha watanzania kupata simu bomba za kisasa kwa bei nafuu.

image[2]Meneja kitengo cha huduma za Internet na simu , James Kagashe (wa kwanza kushoto) akiongea na wateja mbalimbali waliotembelea Airtel Smartphone Bazaar katika eneo la mlimani city kujipatia simu bomba na za kisasa zenye ofa za vifurushi vya muda wa maongezi, sms na intaneti kwa gharama nafuu.

  • Yazindua smartifonika ofa yenye vifurushi vya bure kwa muda wa mienzi 6
  • Wateja kupata ofa za simu za kisasa maeneo ya mlimani city na quality center kuanzia ijumaa hadi Jumapili

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kwa mara nyingine imekuja na ofa kabambe kupitia SMARTFONIKA Bazaar na kuwawezesha wateja kupata simu mbalimbali za kisasa katika msimu huu wa sikukuu

Gulio la simu yaani smartphone Bazaar litakuwa katika maeneo ya Mlimani City na Quality Center kuanzia siku ya Ijumaa, Jumamosi na Jumapili. Watanzania watapata nafasi ya kuchagua na kununua simu za aina ya smartphone inayokidhi mahitaji yao kwa bei nafuu.  Ofa hii pia itapatikana katika maduka ya Airtel  nchi nzima.

Akiongea kwa niaba ya Airtel, Meneja Uhusiano wa Airtel , Jackson Mmbando alisema” Tunayo furaha kutambulisha ofa hii kabambe katika msimu huu wa siku kuu itakayowawezesha wateja wetu kununua simu kwa matumizi yao binafsi na kwaajili ya wapendwa wao kwa bei nafuu kuliko zote sokoni.

Simu zitakazopatikana  katika Smartphone Bazaar ni pamoja na simu aina ya Magnus Bravo Z10 inayokuja na kifurushi cha kuanzia cha bure chenye dakika 150 za kupiga simu, SMS 150 pamoja na kifurushi cha internet chenye ujazo w MB 150 kila mwezi kwa muda wa mienzi 6  kwa gharama ya shilingi 75,000/=.  Magnus Z10 ni simu yenye screen kubwa inayomuwezesha mteja kuona taarifa mbalimbali kwa urahisi zaidi battery yake inadumu kwa muda mrefu

Sambamba na simu ya Magnusa Bravo Z10 wateja wetu watapata simu mbalimbali za kisasa za aina ya Samsung, Huawei, Tecno na Star times ambapo wateja wakinunua watapata ofa kabambe kutoka Airtel.

“Tunaamini simu hizi zitakuwa simu muafaka kwa watumiaji wa mara ya kwanza wa simu aina ya smartphone kuweza kupata uzoefu tofauti na kufurahia huduma mbalimbali ikiwemo huduma ya internet toka Airtel.

Natoa wito kwa wateja wetu kuwa wakwanza kupata simu hizi za kisasa kwa kutembelea maduka yetu na gulio la simu katika maeneo ya mlimani city na Quality center kila mwisho wa wiki.” Aliongeza Mmbando.

Leave A Reply