The House of Favourite Newspapers

Kinamama Waliojifungua Na Watoto Zao Wazawadiwa Bima Za Afya 600 Na Kampeni ya Sambaza Shangwe Gusa Maisha

0
Meneja Mauzo wa Kanda ya Dar es Salaam, George Nyanda akizungumza kwenye hafla hiyo.

Kampuni ya mtandao wa simu za mkononi ya Vodacom imefanya kitendo cha kuirudishia jamii sehemu ya inachokipata kwa kuwazawadia bima za afya 600 watoto waliozaliwa katika Hospitali za Rufaa za Mwananyamala, Amana na Temeke pamoja na mama zao.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, Meneja Mauzo Kanda ya Dar es Salaam George Nyanda amesema;

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mwananyamala akitoa shukrani zake kwa kampuni ya Vodacom kwa wazo lao la kuja kampeni hiyo itakayokwenda kusaidia kuokoa uhai wa mama na mtoto.

“Kwanza napenda niwashukuru wote mliofika kwenye tukio hili ambalo msingi wake mkuu ni kutoa bima za afya kwa watoto waliozaliwa pamoja na mama zao.

“Vodacom kila mwaka tumekuwa na kampeni maalum ya kurejesha kwa jamii sehemu ya tunachokipata ambapo kampeni ya mwaka huu tumeipa jina la “Sambaza Shangwe, Gusa Maisha” tukiamini tunawajibika kabisa kama taasisi ya kibiashara kugusa maisha ya wateja wetu na hata wasio wateja wetu.

“Katika kampeni yetu ya mwaka huu Vodacom tunahakikisha wamama na watoto 200 kwa kila hospitali zinaguswa na kampeni hii.

Kinamama katika wadi ya wazazi Hospitali ya Mwananyamala wakiwa na mfano wa bima ya afya kwenye hafla hiyo. Katikati ni mshereheshaji wa kampeni hiyo Mista Shangwe na kulia kwake ni mmoja wa wauguzi wa hospitali hiyo.

“Hii ni kampeni ya nchi nzima ambapo inatarajia kugusa wahitaji 2000 na mpaka sasa tumeshafanya mikoa tofauti kama vile Mbeya, Zanzibar na leo hii tuko hapa Dar es Salaam ambapo tutakuwa katika Hospitali zetu kuu tatu za kikanda hapa Mwananyala, Amana na Temeke”. Alisema George.

Meneja huyo alimaliza kwa kusema kwa mwaka huu wao kwa kushirikiana na Kampuni ya Bima ya Assemble wameamua kuangalia suala la afya ya mama na mtoto katika kipindi cha kujifungua.

Uongozi wa Hospitali ya Mwananyamala, Amana na Temeke pamoja uongozi wa Vodacom, Mista Shangwe na Essemble Insurance katika picha ya pamoja na mfano wa bima ya afya.

Kwa upande wao Waganga Wafawidhi kutoka Hospital ya Mwananyamala, Amana na Temeke kila mmoja aliishukuru Vodacom kwa kuja na kampeni hiyo iliyoangalia suala la afya ya mama na mtoto ambapo baadhi ya watu wamekuwa wakikosa huduma stahiki kwa kukosa pesa ya matibabu lakini bima hizo zitawasaidia kupata matibabu kwa muda muafaka.

Leave A Reply