The House of Favourite Newspapers

WATU 26 Wafariki Ajali ya Lori na Hiace Mkuranga

Mwonekano wa gari dogo aina ya Hiace T676 DGK baada ya kugongana na lori lililokuwa limebeba chumvi  katika kijiji cha Mparange Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani usiku wa kuamkia leo.
Tela la lori lililokuwa limebeba chumvi likiwa limanguka na kupinduka kando ya barabara baada ya ajali hiyo.
Eneo ambalo magari yaliburuzana baada ya kugongana.
Muonekano wa Hiace kwa pembeni nyuma baada ya kugongana na lori.
Twasira iliyokuwepo eneo la ajali mara baada ya ajali hiyo usiku.

WATU 26 wamefariki dunia na wengine tisa kujeruhiwa baada ya  gari dogo (Hiace) lililokuwa  likitoka Mkuranga kuelekea Kimanzichana mkoani Pwani, kugongana uso kwa uso na lori lililokuwa limebeba chumvi likitokea Mtwara kuelekea Dar es Salaam.

Ajali hiyo imetokea usiku wa kuamkia leo Jumapili Machi 25, 2018 kijiji cha Mparange Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani

Kaimu kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Kibiti, Mohamed Likwata,  amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kwamba majeruhi wote wamepelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam.

Wakati huohuo, Rais John Magufuli amemtumia Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Evarist Ndikilo,  rambirambi kutokana na vifo vya watu 26 vilivyotokea wilayani Mkuruganga.

DK 3 za Dullvan Alivyoamsha Popo Stejini, Dar Live

Comments are closed.