KAMPUNI ya Meta inayomiliki Mitandao ya Instagram na Facebook imetangaza watu wenye tiki za Blue wataanza kulipia malipo yatakuwa Dola 11.99 (Tsh. 27,952) kwa Mwezi au Dola 14.99 (Tsh. 34,945) kwa Watumiaji wa iPhone
Huduma ya malipo itaanza Wiki hii kwa wateja wa Australia na New Zealand ambapo Mtendaji Mkuu wa Meta, Mark Zuckerberg amesema lengo ni kuboresha Usalama kwenye Programu za Mitandao ya Kijamii
Majina ya watumiaji yatalazimika kuendana na yaliyopo katika Kitambulisho cha Mteja na lazima iwepo picha inayoonesha sura ya mhusika.