Waziri Ashatu Kijaji Akabidhi Tuzo Kwa Gf Trucks & Equipment’s Ltd Mkoani Geita
Kampuni ya uuzaji na uunganishaji wa magari na mitambo ya Gf Trucks & Equipment’s Ltd imebuka kampuni ya kwanza inayouza na kusambaza Magari na mitambo ukanda wa mikoa ya kanda ya ziwa.
Hayo yamejiidhirisha wakati wa kufunga maonyesho ya 5 ya teknolojia ya madini mkoani Geita na kuibuka kampuni bora ya usambazaji na uuzaji wa mitambo.
Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo na Waziri wa Viwanda na uwekezaji, Ashatu Kijaji Afisa masoko na mauzo wa kampuni ya GF Poul Msuku alisema wanafurahia kuibuka washindi katika kipengere hicho na wanachukua tuzo hiyo kama chachu ya kujipanga na kuongeza nguvu kaitia uwekezaji kwa kanda ya ziwa
Gf Trucks ambao ni wauzaji wa mitambo na mashine za migodini aina ya XCMG, na magari ya kubebea mizigo ya FAW na Hongyang tuna wateja wengi wanaojiusisha na Uchimbaji wa madini na shudhuli za usafirishaji nchini
Pia Gf waliitumia siku ya kufunga maonyesho kwa kukabidhi Mtambo wa kuchimbia madini kwa mteja aliyenunua katika maonyesho hayo ya madini kwa bei ya punguzo.
Pia Waziri Kijaji aliwataka Gf kuwekeza zaidi katika kwawezesha wachimbaji wadogowadogo ili waweze kujikomboa na kwa kuwawekea utaratibu rahisi kumudu gharama ikiwemo mikopo rahisi na pia aliwataka wachimbaji hao kuchapa kazi itakayoweza kumwongezea kipato na kulipa kodi kwa maendeleo ya nchi.
Naye Mkuurugenzi wa kampuni ya G Unity Squre Ltd, Ezekiel Rembo aliwashukuru GF kwani kwa kushiriki katika maonysho hayo wameweza kununua mashine hiyo (XCMG) kwa gharama nafuu tofauti kama wangeifata Dar essalaam na ameokoa zaidi ya shilling million 10 ikiwamo gharama ya mafuta kuitoa Dar hadi Geita alimaliza .