Waziri Mkuu: Rais Samia Kulihutubia Taifa Aprili 25, 2024
Rais Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kulihutubia Taifa Aprili 25, 2024, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano.
Taarifa hiyo imetolewa mkoani Dar es Salaam na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Aprili 21, 2024 kabla ya kushuhudia safari ya kwanza ya majaribio ya treni ya Reli ya Kisasa (SGR) kutoka Dar hadi Dodoma.
Amesema Rais Samia ameamua kulihutubia Taifa usiku wa Aprili 25 ili kutoa nafasi ya kuendelea kwa ratiba nyingine Aprili 26, 2024, siku ambayo itakuwa ndio kilele cha maadhimisho ya sherehe za Muungano.