The House of Favourite Newspapers

Waziri Nchemba Amtembelea Mama wa Chid Benz

 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba akiwa na mama yake Chid Benz.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba ameguswa na hali ya uathirika wa matumizi ya dawa za kulevya inayomtesa rapa Chid Benz na kulazimika kufika nyumbani kwao kuzungumza na mama yake mzazi.

Chid Benz Abambwa ‘live’ Akibwia Unga, Ndani ya Chumba cha Hoteli

chidi-1-copychidi-4-copy  Picha mbili juu zinamuonyesha Staa wa Bongo Fleva, Rashid Makwilo ‘Chid Benz’, akiandaa madawa kwa ajili ya kuvuta. 

Chid Benz anayemiliki tuzo kadhaa za muziki alijikuta amenasa kwenye mtego wa matumizi ya dawa za kulevya ambao si tu ulimwondoa kwenye maisha ya muziki bali pia uliidhoofisha afya yake na kuuondoa kabisa mwili wake wa ‘chuma’.
Kupitia akaunti yake ya Instagram, Waziri Nchemba ameeleza kusikitishwa na hali ya Chid Benz na kutumia nafasi hiyo kuwataka wale wanaojihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya kuacha mara moja kwani serikali ya awamu ya tano imeazimia kupambana nao.
Hivi ndivyo alivyoandika:
Nimekutana na kufanya mazungumzo na mama wa msanii Rashid Makwilo “Chid Benz” ambaye kwa sasa amepatwa na tatizo la dawa za kulevya.  Inasikitisha na haivumiliki kuona nguvu kazi ya taifa inapotea huku wauzaji wakinufaika kwa pesa haramu.  Ifahamike wazi vita ya serikali dhidi ya magenge, wauzaji na wasambazaji wa madawa ya kulevya imeongezeka hasa katika awamu hii ya tano chini ya Mh. Rais J.P. Magufuli, hivyo anayejihusisha kwa namna yoyote ni vyema akaamua kuachana nayo kabla hajakutwa na mkono wa dola.
 
Mbali ya vyanzo vya taarifa tulivyonavyo, ni wajibu wa kila aliye RAIA MWEMA kutoa taarifa zitakazosaidia kuangamiza biashara haramu ya madawa ya kulevya.
 
Naishukuru familia ya Chid Benz kwa jitihada wanazozifanya kuhakikisha kijana mwenzetu anarejea katika hali yake ya kawaida.
 
Unaweza kuimba, unaweza kufanikiwa, unaweza kutatua matatizo yako bila kutumia madawa ya kulevya.

CHID BENZ Arudia Tena Madawa ,OFM wamnasa Live; Inasikitisha Sana Kwakweli

Comments are closed.