The House of Favourite Newspapers

WEMA ADAI RAHA YA MWANAUME KIPIGO!

Wema Isaac Sepetu

MREMBO wa Bongo Movies, Wema Isaac Sepetu ametoa kali ya aina yake kuwa, katika maisha ya uhusiano, anafurahia kuwa na mwanaume ambaye atampa kipigo kidogo pale anapokosea.

Mwanadada huyo aliyasema hayo hivi karibuni kwenye sherehe ya kuzaliwa ya meneja wake, Neema Ndepanya iliyofanyika nyumbani kwa Wema, Salasala jijini Dar ambapo aliulizwa na Ijumaa Wikienda kuhusu aina ya mwanaume anayependa kuwa naye

ndipo alipotoa ya moyoni.“Napenda mwanaume anipe kipigo kidogo siyo mwanaume mnaishi miaka yote, halafu hata kukupiga kofi kidogo hakupigi,” alisema Wema huku akiangua kicheko cha kiaina.

Comments are closed.