POLISI mkoani Njombe imewakamata watu wawili kwa tuhuma za kuvunja Mahakama ya Wilaya ya Njombe na kuiba vitu mbalimbali ikiwemo sukari, kompyuta mpakato tatu na mashine ya Pos inayotumiwa na mahakama.
Akizungumza na vyombo vya habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Hamis Issa, amesema watu hao ni Masood Mang’ombe na Hamis Ismael na mwingine ni aliyenunua vitu hivyo kutoka Mkoa wa Ruvuma.
Pia amesema wamefanikiwa kukamata mtandao wa watu wanaohusika na wizi wa vifaa mbalimbali kwenye magari zikiwemo taa, maturubai, ekseli na radio.
Kamanda huyo ametoa wito kwa wananchi kufanya kazi halali na kutojihusisha na wizi ili kuepuka matatizo.
Na Amiri Kilagalila, Njombe