WINNIE HARLOW, WIZ KHALIFA SASA MTU NA MKE
MWANAMITINDO, raia wa Canada, Winnie Harlow na rapa Mmarekani, Wiz Khalifa, wameamua kuachia kila kitu nje wakiwaonyesha wote waaotaka kujua kwamba wao sasa ni mtu na mke au mtu na mme.
Hili lilijionyesha waziwazi majuzi jijini Los Angeles, wakati wawili hao walipokuwa wakitoka wameshikana mikono baada ya mechi ya mpira wa kikapu (basketball) kati ya Lakers’ waliochapwa na Rockets na baadaye kutokea vurugu kati ya timu hizo.
Mke wa zamani wa Wiz, mwanamitindo maarufu, Amber Rose, anasemekana ametoa kibali cha wawili hao kusonga mbele.
Si hivyo tu, mastaa hao wamekuwa wakionekana kuwa kwa karibu zaidi kila kukicha.
Comments are closed.