YAJUE MAISA YA UTOTONI YA SNURA
SNURAMWANAMUZIKI wa miondoko ya mduara, Snura Mushi ameifunua siri ambayo wengi hatuijui, eti kwenye makuzi yake alikuwa ni mvivu sana kiasi kwamba kila alipokuwa akitumwa na wazazi wake alikuwa akisingizia kuumwa.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Snura alisema hakuwahi kupenda kutumwatumwa, alikuwa ni mvivu na kila alipoagizwa kufanya jambo alizua ugonjwa wa tumbo ili tu asifanye kazi husika.
“Uvivu huu acheni tu, sasa hivi nikikumbuka najiona mjinga, nilimsumbua sana bibi yangu kwa kusingizia ugonjwa, kila nikiona sasa natumwa naibua ugonjwa ambao sikuwa nao, bibi alinionea huruma na kunitungia jina flani kwani niliumwa kila siku,” alisema Snura ambaye kwa sasa anajituma sana kufanya kazi.
Stori: Hamida Hassan
Comments are closed.