Yanga Walivyotua Songea, Tayari Kuwavaa Majimaji
Wachezaji na viongozi wa Yanga wakati wakiwasili katika Hoteli ya Top One Inn, Songea wakiwa tayari kuwakabili Majimaji.
Mabingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu wa 2015/16 ambao tayari wamekabidhiwa kombe lao Yanga leo watakuwa ugenini katika Uwanja wa Majimaji, Songea mkoani Ruvuma kuwavaa Majimaji.
Mechi hiyo ni mojawapo ya mechi nane zitakazopigwa leo zikiwa ni za kufunga msimu. Mechi nyingine za leo ni pamoja na Simba Vs JKT Ruvu, Azam FC Vs Mgambo JKT, Kagera Sugar Vs Mwadui, Toto Africans Vs Stand United, African Sports Vs Mtibwa Sugar, Mbeya City Vs Ndanda na Tanzania Prisons Vs Coastal Union.