Yanga Yaanza Vizuri, Yaichapa Asas Djibouti 2-0 Klabu Bingwa Afrika – Video
Klabu ya Yanga imepata ushindi wa goli 2 – 0 dhidi ya Klabu ya Asas Djibouti kwenye mchezo wa hatua ya awali ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika
Mchezo huo umechezwa katika Uwanja wa Azam Complex, baada ya Asas Djibouti iliyokuwa mwenyeji kuomba kutumia uwanja huo kutokana na uwanja wao wa nyumbani kukosa sifa
Magoli ya Yanga yamefungwa na Aziz Ki (22′) na Kenedy Musonda (53′). Timu hizo zitarudiana Jumamosi Agosti 26, 2023 ambapo Yanga itakuwa mwenyeji wa mchezo