Yanga Yamtangaza Namba 6 Wake Makudubela Almaarufu ‘Skudu’ – Video
Klabu ya Yanga imethibitisha kumsajili winga Mahlatsi Makudubela almaarufu ‘Skudu’ kwa uhamisho huru kutoka klabu ya Marumo Gallants iliyoshuka daraja huko Afrika Kusini.
Skudu (33) raia wa Afrika Kusini akiwa na Marumo Gallants msimu uliopita alifunga magoli mawili na kutoa asisti 2 kwenye mechi 22.
Skudu anatua klabuni hapo kuchukua jezi namba 6 iliachwa na Feisal Salum aliyetimkia Azam FC.