YANGA YAPIGWA 3-1 NA KAKAMEGA BOYS, YATUPWA NJE SPORTPESA CUP
Timu ya Yanga imeaga kwenye michuano ya Sportpesa Super Cup inayoendelea nchini Kenya baada ya kuchapwa mabao 3-1 na Kakamega Boys kwenye mchezo uliopigwa kwenye Dimba la Ifraha nchini Kenya.
Hii ina maana kuwa Yanga imeaga michuano hiyo baada ya kucheza mchezo mmoja tu, Simba wenyewe watacheza kesho kutafuta ushindi kwenye michuano hiyo.
PICHA: MUSA MTEJA | GPL -KENYA
Comments are closed.