Yanga Yatafuna Miwa ya Mtibwa Manungu
VINARA wa ligi kuu ya NBC Yanga leo imemaliza mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wakata miwa Mtibwa Sugar mchezo ulipigwa kwenye dimba la Manungu Turiani mkoani Morogoro.
Magoli ya Yanga yamefungwa na Sadio Ntibazonkiza kipindi cha kwanza dakika ya 45+5 na Fiston Mayele dakika ya 70 akimalizia pasi safi ya Ntibazonkiza.
Kwa matokeo hayo Yanga imefikisha alama 39 ikiwa kileleni mwa msimamo wa ligi NBC wakiiacha Simba kwa alama nane.