The House of Favourite Newspapers

YONDANI AFUNGUKA KUTOMPA MKONO AJIBU

BEKI mkongwe wa kati wa Yan­ga, Kelvin Y o n d a n i amefuta ukimya na kufungukia ishu yake ya kutopeana mkono na nahod­ha wake, Ibrahim Ajibu.

 

Hiyo, ikiwa ni siku moja tangu iibuke taarifa za wachezaji hao kutokuwepo ka­tika mahusiano mazuri baada ya video kusambaa ya Yondani kukataa kumpa mkono Ajibu.

 

Kitendo hicho kili­tafsiriwa na wengi kuwa Yondani ana kinyongo na Ajibu, baada ya ku­vuliwa unahodha na mikoba yake kukabidhi­wa kiungo huyo.

Tukio hilo la aina yake lilitokea wakati Ajibu akiwatam­bulisha wachezaji wake kwa mgeni rasmi wakati Yanga ilipocheza mchezo wake wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Simba juzi, Dar.

 

Akizungumza na Championi Ju­matatu, Yondani alisema hakuna bifu lolote kati yake na Ajibu huku akitaja uchochezi wa mashabiki ndiyo ume­sababisha minong’ono kuhusu tukio hilo.

 

Yondani amedai kuwa ha­kumpa mkono Ajibu kama masi­hara tu, kwa kuwa siyo utaratibu wa nahodha kushikana mikono na wachezaji wakati akiwatam­bulisha.

 

“Mimi Ajibu ni mdogo wangu na mara nyingi tumekuwa tuki­taniana ndani na nje ya uwanja na hilo tukio la mimi kukataa mkono wa Ajibu nilijua ni masi­hara ananiletea, ndiyo maana nikakataa kumpa mkono.

 

“Kwa sababu Ajibu katika mechi zote za ligi ambazo tume­zicheza hajawahi kutupa mikono wachezaji, yeye anaishia kutut­ambulisha majina yetu na mgeni rasmi ndiyo anatupa mikono, hivyo nashangaa suala hilo lina­vyochukuliwa.

“Kama ningekuwa na bifu au chuki na Ajibu, basi nisingekuwa nampa ushauri na siyo huyo, wachezaji wengi wanafuata ush­auri kwangu kutokana na ukong­we nilionao wakiwemo baadhi Samatta (Mbwana), Msuva (Si­mon) na Banda (Abdi), hivyo niwaondoe hofu mashabiki wa Yanga katika hilo, mimi sina ugo­mvi na Ajibu,” alisema Yondani.

 

Championi Jumatatu, lilimtafuta Ajibu kuzun­gumzia hilo simu yake iliita bila kupokelewa lakini taarifa iliy­osambaa kwenye mitandao ya kijamii ambayo haijathibitishwa kama ni ya Ajibu, inamnukuu hivi:

 

“Nahisi wenzangu walinis­hangaa kuwatambulisha kwa kuwashika mkono, mara nyingi huwa hatufanyagi hivyo, Yon­dani ni kaka yangu na siyo yeye pekee pia Dante (Andrew Vice­nt), Yondani alisita na kuniam­bia hii mpya. Sina shida na kaka yangu huyu, sisi ni wadogo zake na mengi tunajifunza kwake.”

WILBERT MOLANDI, Dar es Salaam.

Comments are closed.