The House of Favourite Newspapers

Zawadi Bora kwa Ndugu ni Bima ya Afya ya Jamii Iliyoboreshwa – HPSS

0

 

Mhariri Mtendaji wa magazeti ya Global Publishers Ltd, Saleh Ally,  kushoto akizungumza na timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) na HPSS Boresha Afya (baadhi hawamo pichani), walipotembelea ofisi za Global Media Group zilizoko Sinza-Mori, Dar es Salaam, ili kutoa elimu na kuhamasisha wananchi kuutumia msimu huu wa sikukuu kutoa zawadi ya Bima ya Afya ya Jamii kwa ndugu na jamaa zao.  Katikati ni Ofisa Uhusiano wa timu hiyo,  Nteghenjwa Hosseah.

TIMU ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) na HPSS Boresha Afya imetembelea  Global Media Group iliyoko Sinza-Mori, jijini Dar es Salaam na kutoa elimu na kuhamisisha wananchi kuutumia msimu huu wa sikukuu kutoa zawadi ya Bima ya Afya ya Jamii kwa ndugu na jamaa zao.

Meneja wa Mradi wa HPSS Tuimarishe Afya, Ally Kebby, akizungumza na +255 Global Radio, aliposisitiza kuwa gharama za kujiunga na bima hii ni sh. 30,000 kwa kaya ya watu sita

Akizungumza katika kipindi cha Front Page kinachorushwa na +255 Global Radio,  Dkt. Boniface Marwa, ambaye ni Mratibu wa Ugharamiaji wa Huduma za Afya wa Tamisemi, amesema Bima ya Afya ya Jamii iliyoboreshwa (iChf) ni Bima ambayo itamwezesha mwananchi kutibiwa kuanzia kwenye zahanati mpaka hospitali za Rufaa za Mkoa kwa gharama ya shilingi elfu thelathini (30,000)  tu.

Timu hiyo ikiwa katika Kitengo cha IT ikipata maelezo kutoka kwa mkuu wake, Edwin Lindege (kulia).

Aliongeza kuwa huduma ambazo mwananchi atazipata kupitia Bima hiyo ni kupata ushauri wa daktari, vipimo vya maabara, vipimo vya picha (x-ray na ultra sound), huduma za matibabu ya macho (isipokuwa miwani au lensi bandia, au jicho bandia), dawa, kulazwa, kujifungua,  huduma za kinywa na meno pamoja na upasuaji (mdogo na mkubwa) kuendana na mwongozo wa matibabu.

 

 

Timu hiyo ikiwa na watangazaji wa kipindi cha Front Page cha +255 Global Radio.  Kushoto ni Lucas Masungwa na Malick Mansour kulia.

 

Leave A Reply