The House of Favourite Newspapers

Zitto Aitaka Serikali Iimilikishe ATCL Ndege Badala ya Kukodi Kutoka Wakala wa Ndege za Serikali

0

Kiongozi mkuu wa Chama cha Upinzani cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amesema utafiti uliofanywa na chama hicho kuhusu Shirika la Ndege la ATCL, unaonesha kwamba mfumo wa umiliki wa ndege za serikali ndiyo unaosababisha shirika hilo lipate hasara.

Zitto amesema kwa mfumo uliopo sasa, ndege zote zinamilikiwa na Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA) ambao ndiyo wanaowakodishia ATCL ndege hizo.

Ameongeza kuwa endapo ATCL ikimilikishwa ndege hizo, hakutakuwa na gharama za kukodi ndege hivyo shirika hilo halitaendelea kupata hasara kama ilivyo hivi sasa.

Leave A Reply