The House of Favourite Newspapers

Zuma Kushtakiwa kwa Kudharau Mahakama

0

MWENYEKITI wa tume ya uchunguzi kuhusu madai ya rushwa yanayomkabili aliyekuwa rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, amesema anataka kiongozi huyo wa zamani ahukumiwe kifungo gerezani kwa kushindwa kufika mahakamani kujibu madai ya ufisadi yanayomkabili.

 

Mahakama ya kikatiba mwezi uliopita, ilitoa uamuzi wake na kusema kuwa Bwana Zuma analazimika kufika mbele ya tume hiyo.

 

Zuma anashutumiwa kuwa wakati wake madarakani, aliruhusu familia tajiri ya Gupta kupora mali za serikali na kushawishi sera na uteuzi wa mawaziri, madai ambayo Zuma anaendelea kukanusha.

Leave A Reply