AKINAMAMA nchini wanatarajia kukutana na kujadili masuala ya kulinda ndoa zao katika kongamano liitwalo VIP Ndoa linalotarajiwa kufanyika Desemba 15 mwaka huu kwenye Jengo la City Mall, Dar.
Akizungumza na wanahabari, mkufunzi wa masuala ya saikolojia na mahusiano, Sadaka Gandi, maarufu kama Anti Sadaka, amesema kutokana na migogoro mingi ya ndoa katika kongamano hilo kina mama watapata somo la kulinda ndoa zao.
Ameongeza kwamba kutakuwa na walimu kutoka Kenya na Burundi ambao nao wataeleza changamoto za ndoa nchini mwao na hivyo kushirikiana kupata utatuzi.
HABARI:NEEMA ADRIAN
PICHA:RICHARD BUKOS/GPL