Tanzia: Mzee Akilimali wa Yanga Afariki Dunia
ALIYEKUWA Katibu wa Baraza la Wazee la Klabu ya Young Africans (Yanga), Mzee Ibrahim Akilimali amefariki dunia leo asubuhi, Jumamosi, Desemba 14, 2019, akiwa Bagamoyo mkoani Pwani.
Uongozi wa Yanga umethibitisha, maziko yatafanyika kesho Jumapili, saa 10 jioni Tandale kwa Mtogole jijini Dar es Salaam.
Endelea kufuatilia taarifa zetu ili kujua taarifa kamili.
Innalilah Wainnailaih Rajiun.