The House of Favourite Newspapers

Mama Diamond Atua Rasmi Bongo Muvi

Sanura Kassim ‘Sandra’,

Na ALLY KATALAMBULA| RISASI MCHANGANYIKO| HABARI

DAR ES SALAAM: Mama mzazi wa staa wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Sanura Kassim ‘Sandra’, ametua rasmi kwenye fani ya uigizaji wa sinema za Kibongo (Bongo Muvi).

Akizungumza na gazeti hili katika mahojiano maalum, mama Diamond alitamba kwenda kimataifa kwenye upande wa filamu kama anavyofanya mwanaye Diamond akiwa ameshiriki katika utayarishaji na uigizaji wa filamu iitwayo Mtepela iliyochezewa huko Kibirizi mkoani Kigoma.

“Nimefanya hiyo filamu na wasanii wa Kigoma, nawajua vizuri lakini kwa sasa siwezi kuizungumzia zaidi,” alisema mama Diamond.

Kwa upande wa mtayarishaji aliyeshirikiana naye aliyejitambulisha kwa jina la Isaya Lazaro almaarufu Zito, alisema mama Diamond mbali na kushiriki katika utayarishaji wa filamu hiyo pia alitoa fedha na ni mmoja wa waigizaji waliofanya vizuri ndani yake.

“Tulimwandalia scene (vipande), akavicheza lakini kabla ya kumaliza alipata safari ya kwenda Afrika Kusini na baada ya kurejea tuendelea kuimalizia”, alisema Zito

 

Shinda Nyumba Awamu ya Pili Yatikisa Jiji La Dar es Salaam

Comments are closed.